Latest in Sports

Music

Home Ads

Monday, December 11, 2017

Mwana FA: Mimi na Jaydee Hakuna Aliyemuomba Msamaha Mwenzake

Mimi na J Dee Hakuna Aliyemuomba Msamaha Mwenzake- Mwana FA
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye hivi karibuni amemaliza tofauti zake na msanii mwenzake Lady Jaydee baada ya kutokuwa na maelewano mazuri kwa muda mrefu, amesema hakuna mtu aliyemuomba msamaha mwenzake kati yao ili kuyamaliza.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Mwana FA amesema ugomvi wake na Jaydee hakuna mtu aliyewakalisha kujaribu kuwapatanisha au wenyewe kuombana msamaha, bali waliumaliza kwa yeye kumpigia simu, na kuzungumza kama ambavyo wengine wanazungumza,


"Hakuna aliyemuomba msamaha mwenzake, mi ndio nilianza, nilimtumia meseji oya vipi, akajibu fresh, nikamwambia FA hapa usiku nilikutafuta, akajibu mimi siku hizi nimezeeka nalala mapema, ndo hivyo tukayamaliza hivyo", amesema Mwana FA.

Mwana FA ambaye kwa sasa ameachia kazi mpya aliyomshirikisha Maua Sama, amesema licha ya kumaliza tofauti zao na Jaydee, watu wasitarajie sana kazi ya pamoja kwani kibinadamu itaonekana wamemaliza tofauti hizo kwa ajili ya kazi.

Monday, September 19, 2016

Ruby: Namuonea hurama Diva, namwombea kwa Mungu amrudishie akili zake!

Baada ya mtangazaji wa Clouds FM, Diva kudai kwamba hamjui msanii wa muziki Ruby, Ruby ameendelea kutema cheche kuhusiana na kauli hiyo.

Muimbaji huyo ambaye ameachana na uongozi wake wa zamani wa THT, ameonyesha kuchukizwa na kauli hiyo ya Diva na kila akiulizwa kuhusu kauli hiyo amekuwa akitoa maneno makali.

“Kuhusu Diva, bora tu niachane naye maana sioni vitu vya kumuongelea kama anavyofanya yeye,” Ruby aliliambia gazeti la Mtanzania “Zaidi namuonea huruma tu, namsikitikia na ninamwombea kwa Mungu amrudishie akili zake. Nahisi ana ugonjwa wa kusahau, jambo ambalo ni baya sana kulingana na umri wake,”

Pia muimbaji huyo amesema kwa sasa amefunga ukurasa wa kuzungumzia masuala ya uongozi wake uliopita kuhu akidai kwa sasa ana nafasi ya kufanya vizuri zaidi kimuziki.

JE Mwanamuziki Billnass Amejiunga na Label ya The Industry ya Nahreel? Jibu Liko Hapa


Msanii na mtayarishaji wa muziki wa The industry, Nahreel ameweka wazi kuwa label ya The industry ina project nyingi na rapper Billnas anayefanya vizuri na wimbo ‘Chafu Pozi’.
billnas

Rapper Billnas hivi karibuni aliwapa taarifa mashabiki wake ujio wa project nyingi kutoka The industry.

Akiongea na Bongo5 Jumamosi hii, Nahreel amesema kwa sasa wana kazi nyingi na rapper huyo.

“Yeah Billnas na The Industry kuna kazi nyingi zinakuja, nisingependa kuziweka wazi kwa sasa kwa sababu ni mapema,” alisema Nahreel. “Lakini pia wasanii wa label ya The Industry tayari wana kolabo nyingi na wasanii wa kubwa hapa nchini, kwa hiyo naweza sema mambo mazuri yanakuja soon,”

Kwa upande wa Kundi la Navy Kenzo, Nahreel amewataka mashabiki wa muziki kukaa mkao wa kula kwa ajili ya ujio wa kazi mpya za kundi hilo.

DUDU Baya a.k.a Mamba Aichana Chana Clouds Fm, Amwagia Sifa Rubby

Msanii mkongwe na asiyesahaulika katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya dudu baya amekivua nguo kituo cha clouds fm kwa kuwaita ni wanafki wakubwa, wanyonyaji wa wasanii, na wenye kuharibia wasanii ndoto za mziki wao
Mamba alitolea mfano wasanii wanazungushwa mikoani kwenye tamasha la fiesta na kuambulia ujira mdogo, huku akisema pesa wanayopata kwenye hilo tamasha huishia hukohuko mikoani na hurudi dar wakiwa wamepayuka hawana kitu mfukoni

Dudu alisema hayo akipokuwa kwenye kipindi cha usiku cha FRIDAY NIGHT LIVE... FNL kinachorushwa na EATV

Alienda mbali zaidi kwa kumpongeza msanii mwenye kipaji anayekuja juu ruby kwa kusema ametoka kwenye minyororo ya wafu FM akawasihi na wasanii wengine wamuige ruby kwani ameonesha mfano

Akionekana mwenye afya km alivyokuwa zamani, amesema wafu fm hawajapiga nyimbo zangu kwa miaka sita sasa lakini sijatetereka naendelea na maisha yangu kama kawaida

Wakati akiendelea kuwatolea uvivu clouds fm mtangazaji wa kipindi hicho sam misago alitumia mbinu ya ziada kumtoa kwenye kile akichokuwa nacho moyoni
Hata hivyo alipongeza redio ambazo zipo chini ya IPP km East africa radio, radio one, capital fm na kusema hajawahi kuombwa pesa na mtangazaji au dj yeyote wa kituo hicho ili wimbo wake uchezwe hewan
Amevitaka vituo vingine kuiga vyombo vya ipp media

Kwa maneno ya dudu baya ni dhahiri wasanii wengi ni watumwa wa baadhi ya media house

Naongoza kwa Kutukanwa Kwenye Muziki, Lakini Najivunia Kuupeleka Muziki Sehemu Fulani – Ruge

Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amesema yeye ni mtu ambaye anaongoza kwa kutukanwa katika tasnia ya muziki kutokana na harakati zake za kuupigania muziki.

Akiongea Ijumaa hii katika semina ya wasanii wachanga wa Dodoma iliyofanyika katika Ukumbi wa Royal Village, Ruge amewataka wasanii hao kuacha kukata tamaa katika harakati wanazopitia.

“Mimi ni mtu ninaeongoza kwa kutukanwa kwenye tasnia ya muziki,” alisema Ruge. “Nimetukanwa sana lakini hilo haliniumizi, najivunia kwa kuwa tumepambana sana kuusimamisha muziki wetu hadi kufika hapa,”.

Ruge Mutahaba ni mmoja kati ya watu waliosaidia kwa namna moja kuchochea kukuwa kwa muziki wa bongofleva nchini licha ya baadhi ya watu kutokubali harakati zake.

Comments system

Disqus Shortname

Powered by Blogger.